Wednesday 6 July 2016

LIONEL MESSI JELA INAMUHUSU

LIONEL MESSI AHUKUMIWA KIFUNGO JELA
Mchezaji mpira wa Argentina na Barcelona Lionel Messi amehukimwa kwenda jela miezi 21 kwa kosa la kukwepa kodi na Hukumu ya aina hiyo hiyo imetolewa na kwa Baba yake, Jorge Horacio Messi.
Aidha kwa Sheria ya Hispania, Hukumu yoyote chini ya miaka 2 inaweza kuahirishwa hivyo basi Mchezaji huyo anawekana asitumikie kufungo hicho. Messi alipofikishwa Mahakamani alijitetea kwa kusema kwamba. ‘Nilikua sina habari ya jambo lolote wakati nacheza mpira, na nilimuamini Baba yangu na Mwanasheria wangu’Alikua anatuhumiwa kwa kuanzisha Makampuni feki huko Belize na Urugwai ili akwepe kulipa kodi ya €4.16m (£3.2m) kati ya mwaka 2007 na 2008.

No comments:

Post a Comment